FM Manyara

Wamiliki wa Vyombo vya moto mkoani Manyara watakiwa kuwa na Bima

June 7, 2024, 2:11 pm

Picha ya maafisa wa polisi kitengo cha usalama Barabarani mkoani Manyara wakitoa elimu katika kituo cha redio cha Fm Manyara

Jeshi la polisi kitengo cha usalama Barabarani Mkoani Manyara kimeendelea kutoa elimu kwa wamiliki wa magari kuwa na Bima za magari ili kuwasaidia wanapopata ajali na kutoa elimu kwa watembea kwa miguu

Na Hawa Rashid

Wamiliki wa vyombo vya moto mkoani manyara wametakiwa  kuvikatia Bima vyombo vyao  vya moto ili kumsaidia mmiliki wa chombo cha moto kifidiwa na bima hiyo pindi anapopata  ajali ikiwemo kuharibika  au kusababisa vifo.

 Wito huo umetolewa na mkaguzi msaidizi wa polisi Henrica Bonifasi kutoka kikosi cha usalama barabarani mkoani Manyara, alipokuwa akizungumza na fm Manyara, amesema kuna aina mbili za Bima ikiwemo Bima ya lawama ambayo nilazima  wamiliki wa vyombo vya moto kuwa nayo kwakua inamsaidia aliyepata  ajali iliyohusishwa  na dereva kumsaidia ,na bima nyinyine ni Bima kubwa inayomsaidia mmliki pindi chombo chake  kinapopata ajali kurudishiwa chombo kipya.

Sauti ya mkaguzi msaidizi wa polisi

kwa  upande wake Koplo Kimbwengo Zacharia kutoka dawati la elimu wilaya ya Babati kitengo cha usalama Barabarani,amesema waathirika wakubwa wa ajali za Barabarani ni watembea kwa miguu na wanawajibu wa kuwapa elimu ya usalama Barabaranii ili kupunguza ajali za Barabarani.

Aidha amesema mtembea  kwa miguu anapaswa kuwa na elimu ya kutosha na kuwa makini anapokuwa Barabani na sehemu sahihi anayotakiwa kuvuka amapokuwa Barabarani ni katika  eneo la kivuko  isipokuwa  eneo la makutano ya Barabara yanapokuwa magari ambapo hapaswi kuvuka.

Koplo Kibwengo Zacharia