FM Manyara

CCM Mkoani Manyara yasikia kilio cha wanachi wa maretadu na labay

May 30, 2024, 6:43 am

Baada ya changamo ya muda mrefu ya kukosa daraja kwa wakazi wa vijiji viwili vya maretadu na labay wilayani Babati mkoani Manyara hatimaye changamoto hiyo imetatuliwa.

Na Emmy Petter

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na Serekali ya mkoa wamezindua daraja la kisasa katika bara bara ya garkawe katika kata ya maretadu lililokuwa na changamoto ya kuvuka  kwa muda mrefu.

Akizungumza baada ya kukagua daraja hilo Meneja wa Tarula wilaya ya mbulu mhandisi Tono Hondo amesema lengo la kujenga daraja hilo la kisasa nikurudisha mawasiliano  kati ya kata ya maretadu na labay kwa kuunganisha kata hiyo na makao makuuu  ya Halmashauri  ya dongobeshi.

Sauti ya mhandisi tono hondo

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Manyara Peter Toima amesema wameridhishwaa na utekelezaji wa mradi huo wa daraja kwa kuzingatia ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM kinachoongozwa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Sauti ya Peter Toima

Aidha, baadhi ya wananchi  wakata hizo mbili wameishukuru serekali kwa kuwa tengenezea daraja hilo kwakua walikuwa wakipata adharaa ya kulala mbali ya nyumba zako kipindi cha mvua pamoja na kushindwa kupeleka mazao yao sokoni nyakati wa mavuno.

Sauti ya wananchi.