FM Manyara

Viongozi wa dini Manyara walia na maadili mabovu

May 20, 2024, 9:18 pm

Picha ya Shekhe Mkuu wa Mkoa Manyara Mohamed Kadidi

Ili kuendelea kuwa na maadili mazuri katika familia, wazazi wametakiwa kuwalinda watoto wao na kuwapa malezi bora kwa kushirikiana na jamii kwa pamoja ili kusaidia kuwa na kizazi bora katika jamii.

Na Hawa Rashid

Viongozi  wa dini mkoani Manyara wameitaka jamii kusimamia vizuri malezi ya watoto wao na maadili mema kuanzia  hatua za makuzi  kwa kuwa hatua hiyo ni muhimu ambapo mtoto anapokuwa mdogo anakuwa mwepesi kuelewa anachofundishwa.

Akizungumza na FM Manyara Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mohamed Kadidi amesema viongozi wa dini  wana nafasi kubwa kwa jamii  kwa kufundisha  masomo maalum ambayo yanapelekea ujenzi wa familia bora  kwa kuwa dini ni mfumo wa maisha  na wazazi  wanapaswa kuwalinda watoto wao  kwa kuwapa chakula, mavazi na mahitaji mengine.

Sauti ya Shekhe Mohamed Kadidi

Kwa upande wake Dkt. Padri Aidan Msafiri ambaye ni Mkurugenzi wa Vijana Jimbo Kuu la Moshi amesema kwa sasa familia nyingi zimekuwa na changamoto kubwa na zenye mzazi mmoja kwa kutengana baina ya familia na shule nyingi ni za kibiashara tofauti na miaka ya nyuma  ambapo kulikuwa na malezi katika shule.

Picha ya padri Aidan Msafiri

Aidha Padri Msafiri amesema kwa sasa jamii imekuwa na ubinafsi kwa kuwa kila mmoja anafikiria mambo yake na hakuna malezi ya pamoja na kusema suala la utandawazi limekuwa na changamoto kwa wazazi kuwapa simu watoto wao. Ameongeza kuwa uwajibikaji wa pamoja unahitajika katika malezi.

Sauti ya Dkt. Padri Aidan Msafiri