Tumbatu FM

Vijana changamkieni fursa za kiuchumi

11 August 2026, 17:05

Picha ya Katibu tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja Ameir Ali Haji (aliesimama) akiwa pamoja na watendaji wa taasisi zavijana zilizopo Kaskazini Unguja kwenye Kongamano la shamrashamra za kuelekea sikuya vijana kitaifa huko Mkokotoni ( Picha na Mwanahwa Hassan)

Serikali zote mbili zimeweka nazingira mazuri kwa makundi ya vijana hivyo ni vyema kuzitumia ipasavyo ili muwezenkujikwamua na hali ngumu ya kimaisha

Na Maulid Juma na Mwanahawa Hassan.

Katibu tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja Ameir Ali Haji amewahimiza vijana kufanya kazi kwa bidii katika kuzikimbilia fursa ziliopo ili kujikomboa kiuchumi na kupata maendeleo.

meyasema  hayo wakati alipokuwa akizungumza na makundi mbalmbali ya vijana wa Mkoa wa Kaskazin Unguja katika kongamano la vijana ikiwa ni  shamra shamra za kuelekea  siku ya vijana duniani huko Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini” A” Unguja.

Amesema kongamano hilo limelenga kuwaunganisha vijana  katika kutoa changamoto zao na kutoa ushauri kwa serikali huku akisema dhamira kuu ni kuhakikisha uelewa unaongezeka na kuwafanya vijana kuzitumia fursa zilizopo.

Sauti ya Katibu tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja akiwa kwenye Kongamanola vijana.

Hata hivyo amesema vijana ndio chemchem ya kuibua watendaji wazuri kwenye serikali na kuchochehea ujengwaji wa jamii iliyobora huku akitoa witokwa vijana kujenga utamaduni mzuri  na  kuepuka vitendo vibaya na hatarishi ambavyo havikubaliki katika jamii.

Ni muendelezo wa sauti ya Katibu tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Kwa upande wake ndugu Abdul- hamid Thabit  Mzee kutoka wakala wa uwezeshaji wananchi kiuchumi Zanzibar (ZEA) amesema kwa mujibu wa shirika la Intergret Labour of servey takwimu zinaonyesha kwa mwaka 2021 asilimia 27.6% ya vijana wa Zanzibar walionekana kuwa    hawana ajira huku takwimu za mwaka 2025 zikionesha kupungua kwa tatizo hilo kwa asilimia 5.4 huku akisema kuwa  wamechukuwa jukumu la kuwapatia mafunzo vijana hao juu ya namna ya kuzifikia fursa ziliopo ili waweze kuajiriwa au kujiajiri na kupata mafanikio.

Awali akisoma risala kwa niaba ya vija wa Kaskazini Unguja Naila Bakari Foum amesema licha  ya kuwa serikali na taasisi mabalimabli za kiraia zinachukuwa juhudi mabalimbali  za kuwajengea uwezo vijana juu ya kuchangamkia fursa ili kujikwamua na umaskin bado Kundi hilo linakabiliwa na changamoto za ucheleweshwaji wa mikopo ukosefu wa mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa fedha kutokuwepo kwa masoko ya uhakika pamojana vikwanzo vinavyoathiri watu wenye ulemavu.

Ni sauti ya Naila Bakari wakati akisoma risala kwenye Kongamano la Vijana Kaskazini Unguja.

Nao baadhi vijana walioshiriki  kongamano hilo wamewaomba vijana wengine kuzikimbilia fursa mbali mbali za kiuchumi zilizopo pamoja na kuwa na moyo wa  kujitolea na kuacha tabia ya kusubiri ajira kutoka serikalini pekee.

Ni sauti za vijana walioshiriki Kongamani lamkuelekea siku ya vijana kitaifa Zanzibar

Kongamano hilo limeandaliwa na Jumuia ya Vijana na Elimu Mkoa wa Kaskazini Unguja(JUVIEKA) kwa kushirikiana na shiriika la ActionAid ambapo kilele cha maadhimisho hayo hufanyika kila ifikapo tarehe  12 Agosti 2026 na kwa mwaka huu Visiwani Zanzibar yatafanyika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa ndege.