Tumbatu FM

Jeshi la polisi lajipanga kudhibiti udhalilishaji kisiwani Tumbatu

3 March 2026, 10:43

Picha ya watendaji wa dawati la jinsia na watoto Mkoa wa Kaskazini Unguja wakiwa kwenye kikao na kamati ya wazazi Skuli ya sekondari Tumbatu. (Picha na Vuai Juma)

“Kunahaja ya kuleta walimu wa usalama wetu kwanza kwaajili ya kutoa elimu kuhusu udhalilishaji kwa shule za Tumbatu ili kuwanusuru watoto na janga hili matukio mengi yamekua yakitokeza ingawa hayaripotiwi”

Na Vuai Juma.

Dawati la jinsia  na watoto Mkoa wa Kaskazini Unguja limepanga kupeleka walimu wa usalama wetu kwanza katika skuli za Tumbatu ili kutoa elimu kuhusu masuala ya udhalilishaji wa kijinsia.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa dawati hilo Inspector wa polisi Salum Khamis Machano wakati wa kikao cha Pamoja kati ya walimu wa skuli ya sekondari Tumbatu Pamoja na kamati ya wazazi kuhusu changamoto ya ukatili wa kijinsia kisiwani humo.

Amesema wamepokea malalmiko kutoka kwa wasamaria wema kuhusu kuwepo kwa baadhi ya watu wa eneo hilo wanaofanya vitendo vya kuwadhalilisha watoto jambo ambalo limewafanya kuweka mikakati itakayopelekea kuliondosha tatizo hilo ikiwemo kuwapeleka polisi watakaosaidiana na walimu kutoa taaluma kwa wanafunzi.

Aidha amewataka wazazi kuwa na tabia ya kufuatilia mienendo ya watoto wao Pamoja na kutowapa uhuru wa kupitiliza jambo ambalo hupelekea kuongezeka kwa matendo mabaya.

Sauti ya mkuu wa dawati la jinsia na watoto Mkoa wa Kaskazini Unguja Sajent Salum Khamis Machano.
Hii ni picha ya mwenyekiti wa kamai ya wazazi skuli ya Tumbatu Ngwali Makame Kire (alie simama) akiwa kwenye kikao na watendaji wa dawati la jinsia na watoto Mkoa wa Kaskazini Unguja. (Picha na Vuai juma)

Kwa upande mwengine mwenyekeiti wa kamati ya wazazi skuli ya sekondari Tumbatu Mwalim Ngwali Makame Kire amaekiri kuwepo kwa vitendo vya udhalilishaji katika
 jamii huku akisema changamoto kubwa ni kutoviripoti kwa mamlaka husika kutokana na ukaribu wa kifamilia.

Ni sauti ya Mwenyekiti wa kamati ya wazazi skuli ya sekondari Tumbatu Mwalim Ngwali Makame Kire.

Nao wajumbe wa kamati hiyo wameliomba jeshi la polisi kuharakisha upatikanaji wa walimu  wa usalama wetu kwanza sambamba na kuipeleka elimu kwa walimu wa madrasa.

Sauti za baadhi ya wajumbe wa kamati ya wazazi Skuli ya sekondari Tumbatu.