Tumbatu FM

Hakikisheni mnafikisha elimu kwa jamii kuhusu utunzaji wa mazingira

22 June 2026, 11:42

Ni picha ya wajumbe wa kamati za Skuli Masheha na Walimu wakuu wakati wa kufunga mafunzo ya mazingira huko ukumbi wa kituo cha walimu TC Mkwajuni Mkoa wa Kasakzaini unguja (Picha na Atka Mosi)

“Fikisheni elimu hii kwa watu mnaowaongoza ndani ya jamii nyinyi ni nguzo muhimu kwenye mapambano dhidi ya upotevu wa uoto wa asili ambao unazidi kutoweka”

Na Atka Mosi Makame.

Mkurugezi wa jumuiya ya vijana na elimu Mkoa wa kaskazini Unguja Mabrouk Maalum Mohamed amewataka masheha walimu wakuu wa skuli na wenyeviti wa kamati za skuli kutuza mazingira yanayowazunguka na kufikisha elimu kwa jamii ili kuepukana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Ameyasema hayo mara baada ya kukamilika kwa mafuzo kuhusu mazingira yaliyofanyika katika ukumbi wa kituo cha walimu TC Mkwajuni Mkoa wa Kaskazini unguja.

 Amesema mabadiliko ya tabia nchi yanatokana na hali ya hewa ya muda mrefu yanasababishwa na uchafuzi wa mazingira kwa ukataji miti,uchimbaji mchanga hali ambayo inapelekea kuengezeka kwa joto.

Amesema lengo la mafuzo hayo ni kutafuta namna ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi hususan katika jamii na mazingira ya skuli huku akisema kuwa washiriki hao wana nafasi kubwa ya kuchangia mabadiliko na kueneza elimu hiyo kwa jamii husika jambo ambalo litasaidia muonekano mzuri na wenye haiba ya kuvutia

Hata hivyo amesema Zanzibar imeanza kushuhudia Athari za mabadiliko ya tabia nchi jambo linalopelekea  kuongezekakwa kina chamabji ya Bahari huku akitowa wito kwa serikali na wanajamii kuendeleza  kudumisha utunzaji wa mazingira.

Sauti ya mkurugezi wa jumuiya ya elimu ya vijana kaskazini Unguja Mabarouk Maalum.

Baadhi ya masheha waliopatiwa mafunzo hayo wameipongeza jumuiya ya JUVIEKA  kwa kuwapatia elimu hiyo na kuahidi kuifanyia kazi kwa kuelimisha watu walio wazunguka  kuhusu madhara ya uharibifu wa mazingira na kuwashajihisha ujuu  ya umuhimu wa upandaji miti.

Sauti za baadhi ya masheha kwenye mkutano wa kufunga mafunzo juu ya utunzaji wa mazingira.

Akizungumza kwa niaba ya wawakilishi kutoka  skuli  zilizoshiriki  mkutano huo   mwalim Bakari Ali kutoka shule ya Mapinduzi sekondari chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja amesema elimu hiyo imekuja wakati muwafaka  na watahakikisha wanaifikisha kwa wanafuzi na wazazi ili kuimarisha uwelewa wa haraka.

Ni mwalim Bakari Ali kutoka shule ya Mapinduzi sekondari chaani.

Nao washiriki wa mafunzo hayo wwameshukuru kupatiwa elimu hiyo na kusema watajitoa katika kuifikisha kwa jamii na kutoa wito kwa vijana kuacha kujitengenezea ajira  zinazotokana na uharibifu wa mazingira.

Ni sauti za wawakilishi wa washiriki kwenye mafunzo ya mazingira huko TC Mkwajuni.

Mafuzo hayo yasiku Mbili  yamesimamiwa na  jumuia ya Vijana na elimu Mkoa wa kaskazini Unguja (JUVIEKA)  kwa ufadhili wa ActionAid ambapo yaliyowashirikisha masheha wenyeviti wa kamati za Skuli  Maafsa Misitu na Walimu wa kuu.