Tumbatu FM

SOS Zanzibar yawafikia wakazi wa shehia ya Jongowe

8 August 2026, 15:38

Ni Picha wa wananchi wa Jongowe Kisiwani Tumbatu wakiwa pamoja na Maafisa wa vitengo mbali mbali kutoka Wilaya ya Kaskazini “A” katika mafunzo yanayotokana na mradi wa IMARISHA FAMILI unaotekelezwa na Taasisi ya SOS Zanzibar (Picha na Mwanahawa Hassan)

“Uwepo wa mashirikiano kati ya masheha kamati za shehia na wananchi ni jambo la muhimu katika kufikia malengo yenu mliyojiwekea nivyema ukamngana pamoja ili mupate mafanikio”

Na Mwanahawa Hassan

Mkurugenzi wa jumuia ya vijana Elimu Mkoa wa Kaskazini unguja ( JUVIEKA) Mbarouku Maalum Mohamed ambae pia msimamizi wa mafunzo katika mradi wa IMARISHA FAMILIA unaotekelezwa na shirika la SOS Zanzibar ameutaka uongozi wa shehia ya Jongowe kushirikiana na wanajamii katika kutekeleza mpango kazi wa maendeleo ya shehia hiyo.

Ameeleza hayo katika ukumbi wa mikutano  wa Chuo cha Mafunzo ya Amali Mkokoton Wilaya ya Kaskazin “A” Unguja mara baada ya kukamilika kwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuaandaa mpango kazi wa maendeleo ya jamii utakaowasaidia katika kutekeleza majukumu yao ili kupata maendeleo.

Amesema mkutano huo umekuwa na mafanikio makubwa kwa wananchi hao kwani umeweza kubainisha rasilimali walizonazo na kuonyesha changamoto mbalimbali zilizopo kwenye jamii yao jambo ambalo amelitaja kuwa ni hatua muhimu ya kuweza kujua namna ya kutekeleza mradi huo.

Nisauti ya 1. ya Mbarouk Maalum ambaye ni Mkurugenzi wa jumuia ya vijana Elimu Mkoa wa Kaskazini unguja pia ni msimamizi wa mafunzo katika mradi wa imarisha familia.

Aidha amewataka wanufaika  wa mafunzo hayo kuwa tayari katika kuzisimamia changamoto walizo zibainisha  ili kuona namna gani wanaweza kuzitatua.

Ni muendelezo wa sauti ya Mbarouk Maalum msimamizi wa mafunzo.

Kwaupande wake Ndugu Othman Hadhir Othman  ambae ni miongoni mwawashiriki wa mafunzo hao amesema amefurahishwa na elimu waliyopatiwa kutokana na umuhimu wake kwani itaweza kuwasaidia wakati wa kutekeleza mpangokazi huo na kupata matokeo mazuri.

Sauti ya ndugu Othman Hadhir Othman  aliyezungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo.

Mafunzo hayo ya siku Tatu (3)  yametolewa  kwa wakazi wapatao 15 kutoka shehia ya Jongowe Pamoja na maafisa mbali mbali wa Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja kwa ufadhili wa shirika la SOS Zanzibar.