Upendo Charity wamfariji Bibi Sabra
8 August 2023, 11:16 AM
Wanakikundi wa Upendo Charity, kinachopatikana katika halamshauri ya Mji wa Masasi mkoani Mtwara, wameshiriki kufanya matendo ya huruma kwa kutoa maziwa ya Lactojeni dazeni moja na nguo za kujikinga na baridi kwa mtoto Sabra aliyezaliwa hivi karibuni katika Hospitali ya Mkomahindo wilaya ya Masasi mkoani Mtwara na kumpoteza mama yake mzazi kwa kufariki hivyo kupelekea mtoto huyo kulelewa na bibi yake anayefahamika kwa jina la Mwajuma Hassani Mkota au Bibi Sabra.
Akizungumza katika tendo hilo la kukabidhi mahitaji hayo mwenyekiti wa kikundi hicho Christine Simo akawa na haya ya kusema…
Kwa upande wake diwani wa kata ya Mkomahindo kilipotokea kisa hicho Ally Salvatori akizungumza katika eneo la tukio pamoja na kuzungumza mengi juu ya faraja waliyotoa kikundi hicho kwa familia ya Bibi Sabra akasema…
Kwa upande wake Bibi Sabra akizungumza katika kutoa shukrani zake aliwashukuru wanakikundi hao kwa moyo wa upendo na ukarimu na kumwomba Mungu awazidishie zaid pale walipotoa wanakikundi hao.