FM Manyara

PSSSF yawanoa maafisa utumishi na wahasibu Manyara

24 February 2026, 6:16 pm

picha ya baadhi ya watumishi na wahasibu wakipatiwa elimu

Mfuko wa Maendeleo ya jamii PSSSF umeendelea kuboresha  huduma  zao  kwa njia ya kidigital kwa kuwafikia maafisa utumishi  na wahasibu katika mikoa kumi kwa kufikisha elimu kwa wanachama wa mfuko huo.

 Na Emmy Peter

Hayo yamesemwa na Meneja wa PSSSF  kanda ya kaskazini Yessaya Mwakifulefule  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo  za hazina zilizoko Mkoani Manyara, amesema mfuko wa PSSF umeendelea kuwaelimisha wafanyakazi  kujiunga na mfuko huo  ili kunufaika kipindi cha uzee.

sauti ya Meneja wa  PSSSF kanda ya kaskazini Yessaya Mwakifulefule
Picha ya Meneja wa  PSSSF kanda ya kaskazini Yessaya Mwakifulefule

 Kwa upande wake  Katibu tawala wa Mkoa wa Manyara Maryamu Muhaji amesema mafunzo hayo yatawasaidia  waajiri pamoja na maafisa utumishi kuwaandaa  watumishi wanaokaribia kustaafu ili kutatua matatizo ya ucheleweshaji wa mafao.

sauti ya Katibu tawala wa Mkoa wa Manyara Maryamu Muhaji

Aidha baadhi ya maafisa rasilimali watu wameushukuru mfuko PSSSF kwa kuwakutanisha  katika mafunzo  hayo na kuwapa elimu kuhusu  mfuko na mafao yatokanayo na mwanachama  ambapo wamesema watahakikisha michango ya mwanachama inakusanywa  na kufikisha  kwa wakati katika mfuko  huo tofauti na ilivyokuwa  awali.