FM Manyara
FM Manyara
17 February 2026, 6:08 pm

Jumla ya makosa 76 yakiwemo makosa ya mauaji ,kubaka na ulawiti yameripotiwa kutokea mkoani Manyara katika ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi wa kumi na moja mwaka jana 2025 hadi mwezi wa pili mwaka huu 2026.
Na George Agustino
Taarifa hiyo imetolewa na kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa manyara Ahmed Makarani alipokuwa akizungumza katika kipindi cha mseto wa leo kinachorushwa na fm Manyara, radio amesema kwa ujumla hali ya usalama ni shwari ndani ya mkoa wa Manyara ambapo ndani ya kipindi hicho makosa 15 ya mauaji, makosa 47 ya kubaka na makosa 14 ya ulawiti ndiyo yaliyokuwa na mshtuko mkubwa katika jamii.
Aidha kamanda Makarani amesema jeshi la polisi kupitia polisi jamii wamekuwa wakishirikiana na jamii moja kwamoja katika kutoa elimu na kupokea taarifa mbalimbali kutoka kwa wananchi zikiwemo taarifa za matukio ya kiuhalifu na kuzifanyia kazi.
