FM Manyara
FM Manyara
12 February 2026, 4:59 pm

Mamlaka ya hali ya hewa mkoa wa Manyara imesema kwa kipindi cha kuanzia mwezi march hadi mwezi mei kunatarajiwa kuwa na mvua za kiwango cha kawaida hadi wastani.
Na Mzidalfa Zaid
Akiongea na fm Manyara meneja wa TMA mkoa wa Manyara Salma Amour amesema kwa mkoa wa Manyara mvua inatarajia kuanza wiki ya pili ya mwezi march hadi mwezi mei na kiwango kikubwa cha mvua kinatarajiwa mwezi april.

Kwa upande wake mtabiri wa hali ya hewa mkoa wa manyara Haji Amimu, amewataka wananchi mkoa wa Manyara wakiwemo wakulima , wafugaji na wavuvi kuzingatia utabiri wa hali ya hewa unaotolewa na TMA ili uwasaidie katika shughuli zao za kila siku.
