FM Manyara

Maafisa usafirishaji Babati watakiwa kufuata sheria za usalama barabarani

29 January 2026, 5:03 pm

Picha ya Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Polisi Wilaya ya Babati, Mrakibu wa Polisi Emmanuel Kandola akiwa na Sajenti wa Polisi Dotto Aloyce kutoka Kikosi cha Usalama Barabarani, Dawati la Elimu

Maafisa usafirishaji maarufu bodaboda pamoja na madereva wengine wa vyombo vya moto wilayani Babati mkoani Manyara wametakiwa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili watumiaji wengine wa barabara waendelee kubaki salama.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa  na mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Mrakibu wa Polisi  Emmanuel Kandolla amesema oparesheni mbali mbali zinaendelea kufanyika kuhakikisha watumiaji wa barabara wanakuwa salama na wanaovunja sheria wanachukuliwa hatua za kuandikiwa tozo au kufikishwa mahakamani .

Sauti ya mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Emmanuel Kandolla

Aidha,Kandolla amesema bado wanaendelea kufanya oparesheni za kuwakamata  na kuwachukulia hatua za kisheria wahalifu ambao wanatumia nafasi za maafisa wasafirishaji nyakati za usiku kupora na kuwaibia watu pamoja na kutenda makosa ya jinai.