FM Manyara

RC Sendiga azindua namba ya huduma kwa mteja Manyara

21 January 2026, 5:29 pm

picha ya Mkuu  wa mkoa wa manyara Queen Sendiga akizindua namba ya bure ya huduma kwa mteja

Mkuu  wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga amezindua namba ya bure ya huduma kwa mteja ambayo itatumika kupokelea  changamoto na kero au malalamiko ya wananchi wote wa mkoa wa Manyara.

Na Mzidalfa Zaid

Sendiga amezindua  namba hiyo ambayo ni 0800787722 na kusema  itasaidia kurahisisha kupokea changamoto nyingi kwa wakati na kuzifanyia kazi  ambapo mwananchi atapiga namba hiyo bure bila malipo au makato yeyote na kutoa  taarifa iliyosahihi  pasipo  kudanganya.

Sauti ya Mkuu  wa mkoa wa manyara Queen Sendiga akizindua namba ya bure ya huduma kwa mteja

Aidha Sendiga  amezitaka ofisi  zote  zilizopo  chini yake kufanyia  kazi kwa haraka na kuzipatia  ufumbuzi changamoto  zote watakazopokea na kurudisha  taarifa katika ofisi ya mkuu wa mkoa ili kutunza  ripoti na taarifa za kila mwezi.  

picha ya Mkuu  wa mkoa wa manyara Queen Sendiga akizindua namba ya bure ya huduma kwa mteja