FM Manyara

Wananchi Babati watakiwa kuchukua tahadhari kipindi cha mvua

5 January 2026, 5:09 pm

Picha ya Mkuu wa jeshi la zima moto na uokoaji wilaya ya Babati mkoani Manyara Emmanuel Kibona

Wananchi wilayani Babati  mkoani Manyara wametakiwa kuchukua taadhari  katika  kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha ili kuepuka madhara yanayoweza  kutokea kutokana na mvua.

Na Mzidalfa Zaid

Taadhari  hiyo imetolewa  leo na Mkuu wa jeshi la zima moto na uokoaji wilaya ya Babati mkoani Manyara Emmanuel Kibona, wakati akiongea na fm Manyara ,amesema wananchi wanapaswa kuchukua taadhari kubwa katika madaraja  yatakayosombwa na maji.

Sauti ya Mkuu wa jeshi la zima moto na uokoaji wilaya ya Babati mkoani Manyara Emmanuel Kibona

Aidha, Kibona amewataka wananchi kutoa taarifa kwa jeshi la zima moto  na uokoaji  kwa kupiga simu bure kwa namba 114 wanapokumbwa  na majanga mbalimbali ikiwemo moto au kuzama maji ili jeshi hilo liweze kutoa msaada kwa uharaka zaidi.