FM Manyara

RC Sendiga awataka wananchi Mbulu kutunza chakula

17 December 2025, 4:57 pm

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen sendiga Amewataka wananchi wa Mkoa wa Manyara kuhifadhi chakula ili kuondokana na bar la njaa wakati wa Mabadiliko ya tabia ya Nchi.

Na Emmy Peter

Sendiga  ameyasema hayo wakati wa ziara yake wilaya ya Mbulu mkoa wa Manyara alipokwa akisikiliza kero za wananchi wa wilaya hiyo na kuzitatua, amesema wananchi  wanapaswa kutunza chakula kwakua mwaka huu hakuna mvua ya kutosha ambapo amesema ni jambo jema kila kaya Kuwa na utaratibu wakuhifadhi  chakula kidogo kidogo.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen sendiga

Aidha, Sendiga amesema njaa ni adui wa maendeleo kwa wananchi hali inayo pelekea  kushuka  kwa utendaji kazi kwa jamii pamoja na  kuzorota kwa uchumi wa kila mmoja pindi linapotokea bar la njaa.