FM Manyara

Mwabulambo awataka wananchi kushiriki zoezi la usafi

28 November 2025, 10:12 pm

Picha ya afisa afya mkoa wa Manyara akishiriki zoezi la usafi

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kushiriki zoezi la usafi katika maeneo yanayowazunguka kama ulivyo utaratibu wa kufanya usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi hapa nchini.

Na Mzidalfa Zaid

Afisa afya mkoa wa Manyara Suten Mwabulambo, amesema halmashauri zote mkoani humo zimejipanga kushiriki zoezi hilo la usafi ambapo litaanza saa kumi na mbili asubuhi hadi saa tatu asubuhi.

Sauti ya Afisa afya mkoa wa Manyara Suten Mwabulambo

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kutunza mazingira kwa kutotupa taka hovyo ili kuweka mazingira katika hali ya usafi.