FM Manyara

Jeshi la polisi Manyara laimarisha usalama kuelekea October 29

28 October 2025, 6:20 pm

Picha ya kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara

Jeshi la polisi mkoani Manyara limesema  kuwa limejipanga kuimarisha  ulinzi na usalama siku ya uchaguzi mkuu ambao unatarajia kufanyika october 29 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake,kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara Ahmed Makarani, amesema jeshi la polisi halitomfumbia macho mtu yeyote atakaeonesha viashiria vya uvunjifu wa amani.

Sauti ya kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara

Aidha,Amewataka wananchi kupiga kura  Kwa amani na utulivu bila kuvunja amani ya nchi , ambapo  amesema mpaka Sasa hakuna matukio ambayo yameripotiwa ya uvunjifu wa amani.