FM Manyara

Ole wao watakaofanya fujo october 29 –RC Sendiga

21 October 2025, 4:52 pm

Picha ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Mkuu wa mkoa wa manyara, Queen Sendiga, amewaonya wananchi mkoani Manyara  kuepuka vitendo vyovyote vinayoashiria  vurugu, uchochezi au uvunjifu wa amani kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba 29 mwaka huu.

Na Mzidalfa Zaid

Sendiga ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ,amesema kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa imejipanga kuhakikisha ulinzi unaimarishwa siku hiyo ya kupiga kura.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa manyara, Queen Sendiga

Aidha,amewaonya watumiaji wa mitandao ya kijamii, hususani kwenye makundi ya whatsapp, kuepuka kusambaza taarifa za uchochezi kwani timu ya mkoa itakuwa na wawakilishi katika makundi  hayo watakaokuja wanafatilia taarifa mbalibali.