FM Manyara

Wananchi Babati watakiwa kujitokeza kupiga kura October 29

20 October 2025, 4:35 pm

Picha ya mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Mkuu wa wilaya ya babati Emmanuela kaganda amewataka wananchi kujitokeza October 29 kupiga kura na kumchagua Kiongozi wanaemtaka atakaeleta maendeleo amani na utulivu.

Na Mzidalfa Zaid

Kaganda ametoa kauli hiyo Leo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, amesema kila mwananchi ana haki ya kupiga kura hivyo ulinzi na usalama utaimarishwa katika maeneo yote ya wilaya ya Babati.

sauti ya mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Amewaonya wananchi wote watakaojaribu kuharibu uchaguzi kwani ni kosa kisheria Kwa mtu yeyote kufanya fujo kati zoezi Zima la upigaji kura, hivyo kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya imejipanga kuhakikisha usalama unakuwepo.