FM Manyara

Wananchi Qash waahidiwa maji na barabara

20 October 2025, 10:38 am

Picha ya mgombea Ubunge jimbo la Babati vijijini kupitia chama cha mapinduzi Daniel Baran Sillo

Wananchi wa kata ya Qash na Vitongoji vyake iliyopo Wilayani Babati mkoani Manyara wameahidiwa maji safi na salama pamoja na ujenzi wa Barabara itakayounganisha maeneo mbali mbali ya kata hiyo na Kata nyingine za jirani.

 Hayo yamebainishwa na mgombea ubunge wa jimbo la uchaguzi la Babati Vijijini kupitia chama cha mapinduzi Daniel Baran Sillo wakati akizungumza na wananchi wa kata Qash waliojitokeza kusikiliza ilani ya uchaguzi katika mkutano wa hadhara.

Sauti ya mgombea ubunge wa jimbo la uchaguzi la Babati Vijijini

Kwa upande wake mgombea udiwani wa kata hiyo Mohamed Issa amesema iwapo atapata ridhaa ya wananchi atashirikiana na mbunge kutatua kero zilizopo kwenye kata hiyo ikiwemo ukosefu wa maji safi na salama, Barabara na umeme kwa baadhi ya Vitongoji kwenye kata ya Qash.

Sauti ya mgombea udiwani wa kata ya Qash Mohamed Issa

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Babati Jackson Haibey ameendelea kuwasisitiza wananchi wa kata hiyo kujitokeza kupiga kura hapo October 29 mwaka huu kwani ni haki yao kikatiba.

Sauti ya Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Babati

Wananchi wa kata ya Qash wakisikiliza ilani na sera za mgombea ubunge jimbo la babati vijijini