FM Manyara

Aldersgate yamlipa mwalimu aliekuwa anadai stahiki zake

19 September 2025, 12:09 pm

Picha ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga akikabidhiwa mkataba wa makubaliano ya malipo kutoka kwa mwakilishi wa shule ya Aldersgate

Kufuatia malalamiko ya Babigumira Sauli, raia wa Uganda, dhidi ya Shule ya Aldersgate,Babati mkoani Manyara akidai mafao yake kwa kipindi alichokuwa akifanya kazi shuleni hapo, hatimae amelipwa stahiki zake zote.
 
 Na Mzidalfa Zaid

Akizungumza mara baada ya kulipwa fedha hizo amesema fedha zote alizokuwa akizidai amelipwa Sauli ameshukuru mkuu wa mkoa wa manyara Queen Sendiga kwa kusaidia kufanikisha  kupata haki yake.

sauti ya Babigumira Sauli

Akiongea kwa niaba ya shule  ya Aldersgate, mwakilishi wa shule hiyo Jacob Simba, amesema maagizo yaliyotolewa na mkuu wa mkoa wa Manyara wameyatekeleza kwa muda mfupi kwa kumlipa mwalimu huyo.

sauti ya mwakilishi wa shule hiyo Jacob Simba

Aidha Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga amewataka wamiliki wa taasisi binafsi kuhakikisha wanalipa wafanyakazi wao mishahara na mafao kwa mujibu wa mikataba ya ajira, akisisitiza kuwa serikali haitavumilia unyanyasaji wa aina yoyote kazini.

sauti ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga