FM Manyara

DC Kaganda awataka wakuu wa idara kutenda haki

16 September 2025, 6:38 pm

picha ya Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda leo amesikiliza na kutatua kero za wananchi ambapo amewataka wakuu wa idara kutenda  haki wanapotatua kero za wananchi.

Na Mzidalfa Zaid

Akizungumza katika viwanja vya stendi ya zamani, Kaganda amesema kazi ya serikali ni kutengeneza mazingira wezeshi ili wananchi waishi  kwa amani na utulivu wakiwa wanshiriki shughuli za maendeleo bila kuonewa.

sauti ya Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Katika  kikao hicho baadhi ya wananchi waliojitokeza katika viwanja hivyo wamelezea kero zao ikiwemo kero ya kudai malipo kutokana na kazi za serikali ambazo walizifanya na hawakupewa stahiki zao, ambapo mwananachi mmoja amedai  fedha alizotengeneza madawati ya shule huku mwananchi mwingine akimdai mkandarasi ambae alikabidhiwa mradi wa REA.

sauti ya wananchi
picha ya baadhi ya wananchi walioleta kero zao

Kufuatia malalamiko hayo, mkuu huyo wa wilaya, ametoa maagizo kwa viongozi husika kuhakisha walalamikaji hao wanapewa stahiki zao na makabidhiano ya pesa hizo yafanyike katika ofisi ya mkuu wa wilaya.

sauti ya Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Aidha, amesema kutakuwa na mwendelezo wa usikilizaji wa  kero za wananchi katika maeneo mbali mbali ya wilaya ya Babati na kesho ataendelea  kusikiliza kero za wananachi katika stendi ya zamani.