FM Manyara

Kanisa la Mungu Tanzania lawataka waumini kushiriki uchaguzi mkuu

20 July 2025, 8:25 pm

picha ya baadhi ya viongozi wa Kanisa la Mungu Tanzania pamoja na wahitimu wa mafunzo ya uchungaji

Waumini wa dhehebu la Kanisa la Mungu Tanzania wametakiwa kushiriki uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika october mwaka huu kwa amani na utulivu na kumchagua kiongozi mwenye sifa ya kuongoza.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa na Profesa Pastory Majembe ambae ni mchungaji mwandamizi wa Kanisa la Mungu Tanzania alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 65 katika shule ya  Kalamu Centla School of Theolgy yaliyofanyika wilayani Babati mkoani Manyara na kuhudhuriwa na waumini wa dhehebu hilo kutoka maeneo mabalimbali ya nchi.

sauti ya Profesa Pastory Majembe ambae ni mchungaji mwandamizi wa Kanisa la Mungu Tanzania

Kwa upande wake Askofu mkuu wa Kanisa la Mungu Tanzania Stephano Sanka, amewataka wahitimu hao kutekeleza yale yote waliyofundishwa shuleni, na kueneza neno la mungu katika makanisa watakayopangiwa kufanya kazi ya kumtumikia Mungu.

sauti ya Askofu mkuu wa Kanisa la Mungu Tanzania Stephano Sanka

Mkuu wa shule hiyo Boniface Majengo ,amewataka watu wote wenye wito wa kumtumikia mungu wafike shuleni hapo ili wapate elimu bora, kwakuwa shule hiyo ina walimu wanaofundisha namna ya kumtumikia Mungu.

sauti ya Mkuu wa shule Boniface Majengo

Nao baadhi ya wahitimu , wamesema kwa kipindi cha miaka mitatu wamejifunza mambo mengi yatakayowasaidia katika maisha yao ikimwemo kumjua Mungu.

sauti ya wahitimu