FM Manyara

TMDA yawaonya wananchi kuuza dawa sehemu za minada

11 July 2025, 10:53 pm

Picha ya dawa

Wafanya biashara wa dawa za mifugo mkoani Manyara wametakiwa kuacha Tabia ya kuuza dawa hizo katika minada au sehemu ambayo haitambuliwi na serikali kwani dawa hizo zinakuwa zimepoteza ubora na ufanisi.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa Leo  na afisa Elimu   Kwa umma na huduma Kwa wateja kutoka Mamlaka ya dawa na vifaa Tiba(TMDA) Kanda ya kaskazini Augustino Malamsha  wakati akiongea na fm Manyara, amesema dawa za mifugo na dawa na binadamu zinauzwa sehemu ambazo zimethibitishwa kuuza bidhaa hizo.

Sauti ya afisa Elimu   Kwa umma na huduma Kwa wateja kutoka Mamlaka ya dawa na vifaa Tiba(TMDA) Kanda ya kaskazini Augustino Malamsha 

Kwa upande wake mkaguzi wa dawa kutoka TMDA Kanda ya kaskazini Benson Mcheza , amewataka wafanyabiashara wa dawa kuzingatia Sheria zilizowekwa Kwa  kuhakikisha kabla dawa hizo hazijaingia sokoni zinathibitishwa.

Aidha, amewataka wananchi kutoa taarifa TMDA wanapobaini uwepo wa wafanyabiashara wa dawa ambao hawana vigezo vya kuuza dawa , ambapo amesema  TMDA inaendelea na ukaguzi wa kuwabaini wafanyabiashara wa namna hiyo.