FM Manyara

E-RITA unavyosaidia wananchi kupata cheti cha kuzaliwa

27 May 2025, 12:42 pm

picha ya viongozi wa RITA wakitoa elimu kuhusu mfumo wa E-RITA

Serikali mkoani Manyara imesema mfumo wa E-RITA unamuwezesha mwananchi kujisajili kwa kiidigital na kurahisisha kupata cheti cha kuzaliwa kwa haraka tofauti na ilivyokuwa awali.

Na Mzidalfa Zaid

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kujisajili kwenye mfumo E-Rita ambao utamuwezesha mwananchi kujisajili kwenye mfumo kupitia njia ya mtandao ikiwemo simu au compyuter.

Wito huo umetolewa na msajili wa vizazi na vifo wilya ya Babati ambaye pia ni mratibu wa wilaya za mkoa wa Manyara  Honest Themba wakati akiongea na Fm Manyara, amesema wanaendelea kutoa elimu hiyo kupitia mikusanyiko ya watu ili watu wajisajili kupitia njia ya mtandao.

msajili wa vizazi na vifo ambaye pia ni mratibu wa wilaya za Babati mkoa wa Manyara  Honest Themba

kwa upande wake msajili msaidizi kutoka ofisi ya Rita wilaya ya Babati Samson Palangyo, amesema ili mwananchi ajisajili  anatakiwa kufuata taratibu zote za usajili kwenye mfumo.

sauti ya msajili msaidizi kutoka ofisi ya Rita wilaya ya Babati Samson Palangyo