FM Manyara

Wahalifu watangaziwa kiama Babati

12 May 2025, 2:16 pm

Picha ya mkuu wa wilaya ya Babati akiongea na wananchi wa kata ya Galapo

Mkuu wa Wilaya ya Babati amezungumza na wananchi wa kata ya Galapo juu ya vitendo vya kihalifu hususani ukatili, huku akiahidi kuanza operesheni maalumu akishirikiana na dawati la jinsia kukomesha vitendo hivyo ambavyo si vya kiungwana na vyakujirudia mara kwa mara.

Na Mzidalifa Zaid

Mkuu wa Wilaya ya Babati Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, ametangaza kuanza kwa oparesheni maalumu dhidi ya makundi yote ya kihalifu, hususan  yanayohujihusha na vitendo vya ukatili katika jamii. 

Kaganda ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Galapo katika mkutano wa hadhara, amesema oparesheni hiyo inalenga kutekeleza kikamilifu ajenda kuu aliyoiasisi tangu alipowasili wilayani Babati ya Amani na maendeleo.”

Sauti ya mkuu wa wilaya Babati

Kwa upande wa  viongozi kutoka dawati la jinsia na watoto wamewataka wananchi kukemea na kutoka taarifa za  ukatili wa kijinsia, pale wanapoona unatendeka au kutokea  na namna ya kutambua viashiria vya ukatili, na umuhimu wa kuripoti mapema kwa mamlaka husika.

Sauti ya kiongozi wa dawati la jinsia Babati