FM Manyara

Waajiri wasiotoa mikataba kuchukuliwa hatua

30 April 2025, 7:34 pm

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga amemwagiza katibu tawala wa mkoa wa Manyara kupita kwenye ofisi za umma na binafsi nakukagua mikataba kwa  wasio na mikataba ili kuchukua hatua kwa waaajiri wanaokwenda kinyume na sheria za kazi hapa nchini

Na Marino Kawishe

Waajiri katika sekta  binafsi mkoani Manyara wametakiwa kuweka mazingira bora ya kazi ikiwa ni pamoja na kuwapatia mikataba wafanyakazi wao na kutatua changamoto mbali mbali zinazowakabili.

Akisoma risala mbele ya mgeni  rasmi kwenye siku ya wafanyakazi duniani mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga, katibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi mkoani Manyara TUCTA Juma Makanyaga amesema kwenye sekta binafsi  ndiko kwenye hali mbaya zaidi.

Sauti ya katibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi mkoani Manyara TUCTA

Akijibu risala hiyo mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga amemwagiza katibu tawala wa mkoa wa Manyara kupita kwenye ofisi za umma na binafsi nakukagua mikataba kwa  wasio na mikataba ili kuchukua hatua kwa waaajiri wanaokwenda kinyume na sheria za kazi hapa nchini.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Aidha, baadhi ya wadau mbalimbali wameiomba serikali kuongez amishahara kwa wafanyakazi ili kuboresha maisha ya wafanyakazi.

Sauti ya wadau