FM Manyara

Mfanyabiashara auawa Manyara               

11 April 2025, 3:30 pm

Mfanyabiashara  mkoani Manyara akutwa ndani ya nyumba yake amefariki baada ya kudaiwa kuuawa kikatili  na watu wasiojulikana kwa kuchinjwa nakitu chenye ncha kali.

Na Mzidalfa Zaid

Mfanyabiashara  maarufu wilayani  Babati mkoani Manyara, Thomas Karatu (48), ameuawa kikatili kwa kuchinjwa  na mwili wake umekutwa ndani ya nyumba yake   katika kata ya Gendi mkoani Manyara.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamesema tukio hilo limetokea April 11 2025 katika mtaa wa Gendi Barazani, ambapo  mwili wa mfanyabiashara huyo umekutwa ndani ya nyumba yake baada ya kudaiwa kuuawa kikatili  na watu wasiojulikana kwa kuchinjwa nakitu chenye ncha kali.

sauti ya mashuhuda

Aidha, Fm Manyara imemtafuta kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara Ahmed Makarani ili kuthibitisha tukio hilo ambapo simu yake imeita bila  mafaniki na juhudi zakumtafuta zinaendelea ili kuthibitisha tukio hilo.