FM Manyara

Manyara kupokea mwenge wa uhuru Julai 12 2025

11 April 2025, 1:12 pm

Picha ya mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga

Viongozi  wa  halmashauri  za mkoa  wa Manyara watakiwa  kuhamasisha  wananchi  kujitokeza kuulaki  mwenge wa uhuru na kufika katika miradi yote itakayopitiwa  na mwenge

Na Mzidalfa Zaid

Mkuu  wa mkoa wa Manyara Queen Cuthbert Sendiga amesema mwenge wa uhuru kwa mkoa wa Manyara unaotarajiwa  kukimbizwa kuanzia tarehe 12 hadi 18 julai mwaka huu katika halmashauri zote za mkoa wa Manyara.

Sendiga ameyasema hayo katika kikao lilichowakutanisha viongozi, wataalamu, na wadau mbalimbali kutoka halmashauri zote za mkoa wa Manyara, ambapo  amesema  maandalizi yote ya kuupokea na kuukimbiza mwenge wa uhuru yamekamilika.

Aidha, Sendiga amewataka viongozi kutoka halmashauri zote za mkoa  wa Manyara kuongeza hamasa kwa wananchi  kujitokeza kuulaki  mwenge wa uhuru na kufika katika miradi yote itakayopitiwa  na mwenge wa uhuru.