FM Manyara

Wananchi Simanjiro, Kiteto na Mbulu boresheni taarifa katika daftari la mpiga kura

September 19, 2024, 5:46 pm

Tume huru ya taifa ya uchaguzi  imewataka wananchi kujitokeza kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura ili kumchagua kiongozi wanaemtaka.

Na Mzidalfa Zaid

Wananchi  wa  wilaya za Simanjiro,Kiteto na Mbulu zilizoko mkoani Manyara wametakiwa kujitokeza kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la mpiga kura  ili wapate kadi ya mpiga kura na kushiriki uchaguzi mdogo na uchaguzi mkuuu.

Hayo yamesemwa leo na mkurugenzi  wa tume huru ya taifa ya uchaguzi ofisi ya Zanzibar  Adam Juma Mkina alipokuwa  akiongea na fm Manyara, amesema watu wenye sifa ya kupiga kura ni wenye miaka 18 na kuendelea au watakaotimiza miaka hiyo mwakani.

Amesema zoezi hilo linawahusu ambao hawakuwahi kujiandikisha, waliopoteza kadi ya mpiga kura,waliohama eno moja kwenda jingine pamoja na wanaotaka kuboresha taarifa zao ambapo amesema zoezi hilo linatarajia kuanza september 25 hadi october 1.

sauti ya mkurugenzi  wa tume huru ya taifa ya uchaguzi ofisi ya Zanzibar  Adam Juma Mkina

Aidha,amewataka wananchi wa wilaya nyingine ambao hawakuhakiki taarifa zao kwa awamu ya kwanza kutokana na sababu mbali mbali wasubiri awamu ya pili ambayo itatolewa na tume.

sauti ya mkurugenzi  wa tume huru ya taifa ya uchaguzi ofisi ya Zanzibar  Adam Juma Mkina