FM Manyara

Wamiliki wa silaha mkoani Manyara watakiwa kuhakiki silaha zao

July 24, 2024, 4:06 pm

Picha ya Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara George Katabazi

Kamanda wa wa polisi mkoani Manyara Geogre Katabazi amesema jeshi la polisi kwa kushirikiana na timu kutoka makao makuu ya polisi Dodoma watafanya uhakiki wa silaa kwa wamiliki wa silaa ili kujiridhisha kama anuani ya mmiliki wa silaa imebadilika na kujiridhisha kama wamiliki wa silaa  bado wapo hai na alama  zinazo itambulisha silaa.

Na. Angela Munuo

Jeshi la polisi mkoani Manyara  limewataka wamiliki wa silaha  mkoani hapa kujitokeza katika vituo vya polisi ili kuhakiki silaha wanazomiliki na kuhuisha taarifa za wamiliki wa silaha kisheria.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara George Katabazi ameyasema hayo julay 23 2024 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, amesema jeshi la polisi kwa kushirikiana na timu kutoka makao makuu ya polisi Dodoma watafanya uhakiki wa silaa kwa wamiliki wa silaa ili kujiridhisha kama anuani ya mmiliki wa silaa imebadilika na kujiridhisha kama wamiliki wa silaa  bado wapo hai na alama  zinazo itambulisha silaa .

Sauti ya Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara

Aidha kamanda Katabazi amewataka wamiliki  wa silaha kuwa makini na silaa wanazotumia  kutobeba silaa wakiwa wamelewa au kuiacha katika mazingira yasiyo sahihi kwakua inaweza kuleta taharuki katika jamii au kuchukuliwa na watu wenye nia ovu na kufanya uhalifu.

Sauti ya Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara