FM Manyara

BoT yazitaka taasisi za kifedha Manyara kujisajili

June 28, 2024, 5:15 pm

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kutokuchukua mikopo kwa wakopeshaji binafsi ili kuondokana na riba kandamizi pamoja na kujua  sheria itakayo mlinda pindi anapochukua mkopo katika Taasisi za kifedha

Na Emmy Peter

Tasisi  za huduma ndogo za fedha zinazokopesha fedha wilayani Babati mkoa  wa Manyara  zimetakiwa kujisajili Bank kuu ya Tanzania BOT ili kupatiwa lesseni za biashara katika hutoaji wa huduma za kifedha kwa wananchi .

Akizungumza katika kikao cha wafanya biashara  watoa huduma ndogo  za fedha kilichofanyaka june  27 2024  katka ukumbi wa White rose wilayani Babati mkoani Manyara, Meneja msaidizi wa huduma ndogo za fedha  kutoka makao makuu ya Bank kuu ya Tanzania BOT Dar es salaam Mary Ngassa amesema wanatoa elimu kwa wakopeshaji  ili wafahamu sheria za ukopeshaji fedha kwa wananchii

Sauti ya Mary Ngassa

Kwa upande wake Afisa biashara mkoa wa Manyara Fue Chedieli amesema kila mkopeshaji  fedha anatakiwa kuwa na lesseni daraja “A” na amewataka wananchi kutokuchukua mikopo kwa wakopeshaji binafsi ili kuondokana na riba kandamizi.

na amewataka kujua  sheria itakayo walinda 

Sauti ya Afisa biashara mkoa wa Manyara

Aidha watoa huduma ndogo  za kifedha wilayani Babati mkoani Manyara wameishukuru Bank kuu ya Tanzania BOT kwa kuwapa elimu hiyo kwakua awali hawakuwa wanajua nakusema itawasaidia  wakopeshaji ambao hawafahamu sheria za ukopeshaji.

Sauti ya watoa huduma ndogo  za kifedha wilayani Babati mkoani Manyara