FM Manyara

Wazazi watakiwa kusimamia ndoto za watoto wao

June 4, 2024, 6:36 pm

Picha ya wanafunzi

Katika kipindi hiki cha likizo kumekuwa na tabia ya wazazi kuwapa watoto kazi nyingi za nyumbani  hali inayopelekea watoto kusahau walichofundishwa shule nakushindwa kutimiza ndoto zao

Na Marino Kawishe.

Wazazi na walezi wilayani Babati mkoani Manyara wametakiwa kuendelea kuwasisimamia watoto wao katika kipindi hiki cha likizo ili wajisome badala ya kuwatumikisha na shughuli  za nyumbani

Wito huo umetolewa na Afisa elimu msingi Halmashauri ya wilaya ya Babati mkoani hapa Getrude Kavishe alipokuwa akiongea na Fm Manyara, amesema katika kipindi hiki cha likizo kumekuwa na tabia ya wazazi kuwapa watoto kazi nyingi za nyumbani hali inayopelekea watoto kusahau walichofundishwa shule.

Sauti ya Afisa elimu msingi

kwa upande wake Afisa elimu kata ya endakiso Milikiori Gobre amesema wamekuwa wakiweka muda waziada  kwa kwatoto kujisomea ili kuendelea kukuza uelewa wao ambapo amewataka wazazi kuwapa nafasi watoto wao katika masomo ikiwemo kuonyesha  ubunifu na kuwapa muda wa kujifunza kufanya shughuli mbali mbali  za kiubunifu .

Sauti ya Afisa elimu kata ya endakiso.

AidhaMkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Babati Anna Mbogo amewataka  watoto  kuzingatia wanayofundishwa ili kutimiza ndoto zao kwakua zinaanzia utotoni hadi  kufikia malengo yao ikiwemo kuwa marubani na madakta.

Sauti ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Babati.