FM Manyara

Pelekeni watoto wa kike shule Manyara

May 20, 2024, 11:53 am

Picha ya Mkuu wa mkoa wa Manyara katikati akiwa anakata utepe

Jamii za kifugaji mkoani Manyara zimekiwa kucha tabia ya kumuozesha mtoto wa kike na badala yake kumpa elimu ambayo itamsadia kwakua anamchango mkubwa katika jamii.

Na Angela Munuo

Wazazi na walezi wa jamii ya kimasai wilayani Simanjiro  mkoani Manyara wametakiwa kuona umuhimu kuwapatia elimu watoto wa kike kwakua binti anapofanikiwa kupata kazi anamsaada mkubwa kwa familia na jamii kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga alipokuwa akiweka jiwe la msingi katika chuo cha wanawake na vijana cha Icrate Foundation katika kijiji cha endoret  wilayani Simanjiro mkoani Manyara,ambapo amewataka wazazi kuachana na tabia ya kuwaozesha watoto wakike na badala yake kuwaacha wapate elimu.

Sauti ya Rc. Queen Sendiga

kwa upande wa wanafunzi walioshindwa kuendelea na masomo kutokana na sababu mbali mbali wanaosoma kwenye chuo hicho wamelishukuru shirika la Icrate foundation kwa kufanikisha mradi huo ambo utawasaidia watoto wa kike kujikukwamua kiuchumi kutokana na mafunzo wanayoyapata ya ujasiriamali yanayofundishwa chuoni hapo.

Sauti ya Wanafunzi