Butiama FM Radio
Butiama FM Radio
27 August 2026, 8:34 pm

Ninawasihi wananchi wote wa Mkoa wa Mara kuhakikisha watoto wao walio chini ya umri wa miaka 10 wanapata chanjo ya polio, Chanjo hii ni muhimu katika kuwalinda watoto dhidi ya ugonjwa huu na madhara yake, ikiwemo ulemavu.” Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanal Evance Mtambi.
Na Amos Marwa
Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 27 Agosti, 2026 amezindua zoezi la ugawaji wa chanjo ya polio kwa watoto chini ya miaka 10 uliofanyika katika Shule ya Msingi Butiama A, Wilayani Butiama.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mtambi amewataka wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa afya ili watoto wote wapate chanjo itakayowakinga dhidi ya ugonjwa wa polio.

Mtambi amewahakikishia wazazi, walezi na wananchi wote kuwa chanjo hiyo ni salama, haina madhara na inasaidia kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa polio.
Katika awamu hii, jumla ya watoto 1,048,727 wanatarajiwa kupatiwa matone ya chanjo ya polio katika Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara kuanzia leo tarehe 27 Agosti, 2026 hadi tarehe 30 Agosti, 2026.
