Butiama FM Radio

Vilevile cup yawasha moto Butiama

1 July 2026, 9:15 am

Wanakamati wa mshindano ya Vilevile Cup ambao ni familia ya Mzee wa Jackton Nyambeleka Nyerere, wakiwa katika uzinduzi wa mashindano hayo. picha na Amos Marwa

Timu zilizothibitisha kushiriki mashindano ya Vilevile Cup mwaka huu zimegawanywa katika makundi mawili. Kundi A linaundwa na Bisarye FC, Kigori FC, Muriaza FC na Rwamkoma FC, huku Kundi B likijumuisha Toto Tundu FC, Ikorokomyo FC, Bumangi FC, Vijana Muriaza FC na Bodaboda FC. Mashindano yatafunguliwa rasmi Julai 4, 2026, kwa mchezo wa ufunguzi utakaowakutanisha Bisarye FC dhidi ya Mtuzu FC kwenye Uwanja wa Mwenge uliopo Butiama. Baada ya kuhitimishwa kwa mashindano hayo, bingwa atakabidhiwa kombe na medali, mshindi wa pili atazawadiwa medali, mshindi wa tatu pia atapata medali, huku mchezaji bora wa mashindano, golikipa bora na kocha bora wakitunukiwa tuzo maalum” Kulwa Karedia Jackton mratibu wa mashindano

Na Amos Marwa

Mashindano ya Vilevile Cup, yanayofanyika kila mwaka Wilaya ya Butiama kwa lengo la kuthamini na kutambua mchango wa Jackton Nyambeleka Nyerere, yamezinduliwa rasmi leo, Juni 30, na Kamati ya Maandalizi ya mashindano hayo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mratibu wa mashindano hayo, Kulwa Karedia Jackton, ambaye ni mwanafamilia wa Jackton Nyambeleka Nyerere, amesema lengo la mashindano hayo ni kukuza vipaji vya vijana, kuzuia vitendo vya uhalifu, pamoja na kuimarisha amani, upendo na mshikamano katika jamii.

Sauti ya Mratibu wa mashindano hayo, Kulwa Karedia Jackton, akielezea maandalizi ya mashindano hayo
Mratibu wa mashindano ya vilevile cup, Kulwa Karedia Jackton akitoa maelezo mafupi kwa washiriki wa mashindano muda mchache kabla ya kuzindua rasmi mashindao hayo. Picha na Amos Marwa

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wa mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza Julai 4, wamewashukuru waandaaji kwa kuendelea kuandaa mashindano yanayowapa vijana fursa ya kuonesha vipaji vyao, huku yakichochea umoja na ushirikiano katika jamii.

Sauti ya baadhi ya washiriki wa mashindano hayo wakitoa pongezi kwa wandaaji na kusema kuwa mashindano hayo ni chachu kwao kuonyesha vipaji vyao

Wakati huo huo, Kamati ya Maandalizi imezitaka timu zote zitakazoshiriki kuzingatia nidhamu ndani na nje ya uwanja ili kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa amani, ushindani wa haki na mafanikio.

Jezi zitakazotumika na timu zitakazoshiriki katika mashindano ya vilevile cup 20206. picha na Amos Marwa