Butiama FM Radio
Butiama FM Radio
18 April 2026, 11:20 am

Kuna aina nyingi za uhalifu ikiwemo uhalifu dhidi ya mali, uhalifu dhidi ya binadamu, uhalifu dhidi ya maadili ya jamii yetu na uhalifu wa kimtandao hizo zote zinasumbua jamii.
Na Oscar Mwakipesile
Jamii Wilaya ya Butiama imepewa elimu kuhusu uhalifu na namna nzuri ya kukabiliana na uhalifu katika jamii ili kwendeleza amani katika jamii.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa opareshioni wilaya ya Butiama Asp Laban Akeyo alipozungumza kupitia Butiama FM katika kipindi maalumu na kusema kuwa ukosefu wa ajira na vijana kutamani kuwa na maisha mazuri kwa kuiga maisha mitandaoni kumechochea kuongezeka Kwa uhalifu katika jamii na kuelezea viashiria mbalimbali ambavyo wananchi wanaweza kuvitambua ili Kupunguza uhalifu huku akielezea aina mbalimbali za uhalifu.