Radio Fadhila

Wakazi Masasi wasisitizwa chanjo kwa  wanyama wanaofugwa

26 August 2025, 7:53 PM

Mbwa akipatiwa chanjo. Picha na Public Health Blog

Tukichanja  mbwa wetu, siku  akikung’ata  kutakuwa  na  madhara  ya  kawaida, tuhakikishe  mbwa  wanachanjwa ili kuepuka  ugonjwa  hatari  wa  kichaa cha mbwa

Na Neema Nandonde

Mkuu  wa  Wilaya  ya Masasi  mkoani Mtwara, Rachel  Kassanda  amewataka  wakazi wa  wilaya  hiyo  kuwapa  chanjo  wanyama  wanaofugwa,  ili kuepuka  magonjwa  yanayosababishwa  na  wanyama  hao ikiwemo kichaa  cha mbwa.

Ameyasema  hayo  Agosti 26, 2025 alipokuwa  akizungumza  katika kikao  cha  tathmini ya  utekelezaji  wa mkataba  wa lishe ngazi  ya  jamii kwa  robo ya  nne ya  mwaka 2024/2025,  kilichofanyika  katika  ukumbi wa  halmashauri ya  wilaya  Masasi.

Sauti ya Mkuu  wa  Wilaya  ya Masasi  Rachel  Kassanda

Kwa upande  wake Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri  ya  wilaya  ya  Masasi  Alphaxad Etanga,  amewasisitiza  wajumbe  wa  kamati  ya  lishe wilayani  humo kuhakikisha  kuwa wanaendelea kuhamasisha  jamii kuhusu umuhimu wa  lishe  bora,  huku akisisitiza kuwa kuchangia  chakula cha mchana  kwa  wanafunzi shuleni ni lazima.

Aidha  amewaomba  viongozi  wa  dini kufikisha ujumbe kwa  waumini wao,  kuhusu umuhimu  wa kuwapeleka watoto ili kupata  chanjo  ya ugonjwa wa polio.

Sauti ya Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri  ya  wilaya  ya  Masasi  Alphaxad Etanga