FM Manyara

TGNP Manyara yamsaidia mzee aliyetelekezewa watoto

2 October 2024, 9:01 pm

Picha ya wanachama wa Kituo cha Taarifa na Maarifa  wakimsaidia kujenga nyumba mpya mzee aliyetelekezewa watoto na mke wake

Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP Mkoani Manyara umemsaidia mzee Tlaho Meho kumjengea nyumba kwakua mazingira anayoishi ni hatarishi kwake na watoto wadogo alioachiwa na mke wake aliyemtoroka.

Na Marino Kaweshe

Kituo cha Taarifa na Maarifa  kinachofanya kazi zake kwenye kata ya Mamire wilayani Babati mkoani Manyara kimesema licha ya changamoto za kukosa ushirikiano kutoka kwa baadhi ya wananchi kitaendelea kuzisaidia jamii za watu masikini na  wasiojiweza.

Akizungumza na FM Manyara, Mratibu wa Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP mkoani Manyara Clara Malley amesema miongoni mwa kazi wanazofanya ni kumjengea nyumba ya kuishi mwananchi mmoja ambaye makazi yake ni duni na huku akitelekezewa watoto wawili na mke wake ambaye amekimbia familia hiyo zaidi ya miezi mitatu sasa.

Sauti ya mratibu wa Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP Mkoani Manyara

Kwa upande wake Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto  mkoani Manyara  WP Leokadia akizungumza na wanakikundi hicho cha taarifa na maarifa kutoka kata ya Mamire amesesitiza wananchi kuripoti matukio ya ukatili ambayo yanafanywa kwenye maeneo wanayotoka.

Sauti ya Mwakilishi wa dawati la jinsia na watoto  mkoa wa Manyara 
picha ya Mwakilishi wa dawati la jinsia na watoto  mkoani Manyara  WP Leokadia akizungumza na wannchi wa kitongoji cha Gubali

Kituo cha taarifa na maarifa cha mamire kipo katika hatua za awali kukamilisha ujenzi wa nyumba yenye chumba na sebule kwa mkazi wa kitongoji cha Gubuli katika kijiji cha Endagile kwenye kata ya mamire ambaye makazi yake ni duni na hayana hadhi ya kuishi binadamu.