Buha FM Radio
Buha FM Radio
21 June 2026, 2:14 pm

Wananchi wilayani Kasulu wahimizwa kujiunga katika Chama Cha Msalaba Mwekundu kikitajwa kuwa kina mchango mkubwa katika jamii.
Na; Emily Adam
Chama cha Msalaba Mwekundu Redcross Tawi la Mjini na Mrusi, Halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma kimefanya uchaguzi wa viongozi katika nafasi mabimbali wakiwemo Mwenyekiti, Mwakilishi wa vijana pamoja na wanawake na kuahidi kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa baina yao na wanachama ili kufanikisha malengo ya chama hicho.
Uchaguzi huo umefanyika shule ya msingi Kasulu ambapo baada ya Wilibroad John Mlazi kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa tawi la Kasulu Mjini amewashukuru wanachama kwa kumchagua kwa kura zote kuahidi kuwa atafanya kazi kwa waledi kama katiba yao inavyoelekeza.
Aidha amesema Redcross ina lengo la kuhudumia jamii kwa kushirikiana na serikali katika majanga mbalimbali kama vile mlipuko ya magonjwa pamoja na mambo mengine.
Kwa upande wake mwenyekiti wa tawi la mrusi Anjero Prosper Tungalaza ametoa wito kwa wananchi kutambua mchango wa Redcross katika maeneo yao na kujiunga na chama hicho kwani kina umuhimu mkubwa katika jamii.
Katika hatua nyingine Mwakilishi wa wanawake Justina Elisha Chija na mwakilishi wa vijana Issack Ntacho wamesema chama cha msalaba mwekundu Redcross kimekuwa mkombozi kwa wanawake hasa wajawazito wanaojifungua na kupoteza damu nyingi pamoja na wahanga wa ajali kwa kujitolewa damu kwa asilimia kubwa.
Jumla ya wanachama 24 wa Msalaba Mwekundu Tawi la Kasulu Mjini na 20 kutoka Mrusi wameshiriki katika kuchagua viongozi hao ambao wataendelea kutoa ushirikiano ili kuimarisha na kudumisha chama hicho chenye mchango mkubwa ndani ya jamii na taifa kwa ujumla.