Buha FM Radio

TAWEN kuwawezesha kiuchumi wakazi wa Kasulu

6 June 2026, 5:05 pm

Baadhi ya washiriki wa semina ya TAWEN iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Kasulu. Picha na Irene Charles.

Shirika la TAWEN limesema limejipanga kuwawezesha wananwake wa Halmashauri ya Mji Kasulu kiuchumi na kuachana na vikundi vya vikomba ambavyo vimekuwa changamoto kwa baadhi familia.

Na; Irene Cherles

Katibu Tawala Halmashauri Mji Kasulu Bi.Theresia Mtewele amesema elimu ya ujasiriamali ndio ufunguo wa kukabiliana na umasikini akitaja kuwa Selikari imefungua milango mingi ya kiuchumi kwa wananchi wake.

Akizungumza katika halfla ya uzinduzi wa TAWEN (Tanzania Women Empowerment Network) mkoa wa kigoma  ulioambatana na  semina ya nishati safi  ya kupikia pamoja na elimu ya ujasiliamali Theresia  amesema Mafunzo hayo yamekuja kufungua njia na kuvutia wadau wengi  kwaajili ya kuleta maarifa kutokana na rasilimali zilizopo.

Sauti ya Katibu Tawala wilaya ya Kasulu.

Aidha amevisistiza vikundi vya wanawake na vijana kutofanya biashara kwa mazoea bali waunde vikundi rasmi na kujisaji katika Halmashauri au ofisi za kibenki kwa lengo la kupata mitaji.

Sauti ya Katibu Tawala wilaya ya Kasulu.
Katibu Tawala Halmashauri Mji Kasulu Bi.Theresia Mtewele wakati akizungumza katika hafla ya TAWEN. Picha na Irene Charles.

Kwa upande wake mwenyekiti wa wa TAWEN Bi. Silesi Mali amesema maono TAWEN ni kuwawezesha wanawake na vijana kiuchumi kwa kuwaonesha fursa zilipo ndani ya Wilaya ya Kasulu pamoja na kuwapatia elimu ya kuendeleza miradi inayotokana na fursa hizo.

Sauti ya Mwenyekiti wa wa TAWEN Bi. Silesi Mali.

Katika hatua nyingine Mali amesema changamoto kubwa iliyopo kwa sasa wanawake wengi wameegemea kwenye vikoba ambavyo vimesababisha migogoro katika familia huku akiwasisitiza wananchi watakaofika TAWEN wawe na wazo la biashara ya kufanya.

Sauti ya Mwenyekiti wa wa TAWEN Bi. Silesi Mali.
Sauti ya Mwenyekiti wa wa TAWEN Bi. Silesi Mali wakati akizungumza na washiriki wa semina ya TAWEN. Picha na Irene Charlse.

Kwa upande wao baadhi ya washiriki wamesema kupitia semina hiyo wamejifunza vitu vingi huku wakiomba Selikari kuendelea kutoa elimu juu ya upataji wa mikopo pamoja na matumizi sahihi ya nishati safi.

Sauti za washiriki wa semina ya TAWEN.

TAWEN ina jukumu la kutoa taarifa za kibiashara, maonesho, uandaji wa makongamano lengo ni kuwajengea uwezo Wanawake kupitia mafunzo mbalimbali pamoja na kuwapatia masoko yenye uhakika.