Radio Fadhila

CCM Masasi mguu sawa ujio wa Dkt Samia

22 September 2025, 7:50 PM

Baadhi ya maeneo ya Masasi yakiwa yamepambwa na mabango yanayoashiria kumpokea Mgombea Urais kupitia CCM Dkt Samia Suluhu Hassan. Picha na Godbless Lucius

Kama  wana  Masasi jumanne ya  septemba 23, 2025 tuna  kila  sababu  ya  kwenda  kumsikiliza mgombea urais  kupitia  Chama  Cha Mapinduzi, maana kuna  mengi mazuri ameyatenda  kwetu

Na Neema Nandonde

Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya  Masasi  mkoani Mtwara kimesema  kimejipanga ipasavyo kwaajili ya  ziara  ya  mgombea urais  kupitia  chama  hicho ambaye pia  ni Rais  wa  Jamhuri  ya  Muungano wa Tanzania  Dkt Samia  Suluhu  Hassan siku ya septemba 23, 2025.

Katibu mwenezi CCM wilaya ya  Masasi  Twahili Said  Mayola, ameyasema  hayo septemba 22, 2025, alipokuwa  anazungumzia ujio wa Dkt Samia  kwenye  kipindi  cha Stendi  Kuu kinachorushwa  na  redio Fadhila.

Aidha  amewataka  wakazi  wa  wilaya  hiyo  kujitokeza  kwa  wingi kwenye  mkutano mkubwa wa hadhara  utakaoongozwa na Dkt Samia utakaofanyika kwenye  uwanja  wa  Boma,  ili wasikilize sera  na  mipango  chanya ya  Chama  cha  Mapinduzi  kwa  miaka mitano ijayo.

Sauti ya Katibu mwenezi CCM wilaya ya  Masasi  Twahili Said  Mayola
Katibu mwenezi CCM wilaya ya  Masasi  Twahili Said  Mayola akizungumza na wananchi kupitia redio Fadhila. Picha na Wito Mbwilo

Sambamba  na  hayo  Mayola amesisitiza  kuwa,  kutokana  na kazi  kubwa  ya  kuleta  maendeleo nchini ikiwemo wilayani Masasi, iliyofanywa  na  serikali  inayoongozwa  na  Dkt Samia, wakazi  wa  Masasi wana kila  sababu  ya kufurahia  maendeleo  hayo na kuunga  mkono  jitihada  zilizofanywa na  serikali hiyo kwa  kumchagua tena Dkt Samia.

Sauti ya Katibu mwenezi CCM wilaya ya  Masasi  Twahili Said  Mayola

Mgombea urais  kupitia  chama Cha Mapinduzi Dkt Samia  Suluhu  Hassan ataanza rasmi ziara mkoani Mtwara siku ya  septemba 23, 2025  hadi septemba 26, 2025 ambapo atafanya mikutano ya kampeni kwenye maeneo mbalimbali, ikiwemo Uwanja wa Boma wilayani Masasi.

Katibu mwenezi CCM wilaya ya  Masasi  Twahili Said  Mayola akizungumza na wananchi kupitia redio Fadhila. Picha na Wito Mbwilo