Radio Fadhila

Makala aijibu CHADEMA kuhusu makaa  ya  mawe

19 April 2025, 11:44 AM

Katibu wa NEC, itikadi, uenezi na mafunzo CCM taifa,  CPA Amos Makala akihutubia wanachama na wananchi wilayani Masasi. Picha na Godbless Lucius

Si kila   gari lililobeba  makaa  ya  mawe ni kwaajili  ya kusafirisha  kwenda  kuuza nje  ya nchi, kuna  viwanda  vingi nchini vinatumia  makaa  ya  mawe  ikiwemo  kiwanda  cha  saruji cha Dangote kilichopo mkoani Mtwara.

Na Neema Nandonde

Katibu wa NEC, itikadi, uenezi na mafunzo CCM taifa  CPA Amos Makala amesema kuwa si makaa  yote  ya  mawe  yanasafirishwa  kwenda kuuzwa  nje, bali   mengine  yanasafirishwa  kwenda  kwenye  viwanda mbalimbali  vilivyopo nchini ikiwemo kiwanda  cha  saruji  cha  Dangote  kilichopo mkoani Mtwara.

Akizungumza katika  mkutano wa  hadhara April 17, 2025 na  wananchi  wa  wilaya  ya  Masasi katika  viwanja  vya  Sabasaba  ikiwa  ni hitimisho  la  ziara  ya  siku 10 kwenye  mikoa  ya  Lindi na  Mtwara, MAKALA  amesema  kuwa hata  kuuza  makaa  ya  mawe nje ya nchi ambako kuna uhitaji mkubwa si  haramu, kwani  inasaidia  kupata  fedha  ambazo zinaendeshea  miradi mbalimbali ya  maendeleo.

Sauti ya CPA Amos Makala kuhusu makaa ya mawe

Aidha emeeleza  kuwa, kuruhusu  wawekezaji   kwenye miradi mikubwa ya serikali  ikiwemo bandari, ni njia  moja wapo ya  kuboresha utendaji kazi  wa miradi  hiyo, akitolea  mfano  bandari  ya  Dar-es-salaam ambayo utendaji kazi  wake  kwa  sasa  umeboreshwa kwa kiasi  kikubwa  toka ikabidhiwa  kwa  DP World.

Sauti ya CPA Amos Makala kuhusu bandari

Ikumbukwe kuwa kwenye ziara  ya hivi karibuni ya viongozi wa  Chama  cha  Demokrasia  na  Maendeleo  (CHADEMA) kwa mikoa ya ya kusini,  miongoni mwa yaliyozungumzwa  ni kile walichoeleza  kuwa  licha  ya  mkoa wa Ruvuma  kuzalisha  makaa  ya  mawe,  hawanufaiki  ipasavyo na malighafi hiyo ambayo husafirishwa kwa wingi kwenda kuuzwa  nje ya  nchi.