Radio Fadhila

DC Masasi ahimiza jitihada zaidi kuinua kiwango cha elimu

11 April 2025, 2:26 PM

Mkuu wa wilaya ya Masasi Bi. Rachel Kassanda akifuatilia baadhi ya matukio yaliyokuwa yanaendelea wakati wa mkutano wa hadhara. Picha na Godbless Lucius

Wanafunzi waliotakiwa  kujiunga  na  kidato cha kwanza mwaka 2025, asilimia 98 wamesharipoti shuleni na kuanza masomo.

Na Neema Nandonde

Mkuu wa wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Bi. RACHEL KASSANDA, amewataka wakazi wa wilaya  hiyo kuzidisha  jitihada  katika  kuinua  kiwango cha elimu.

Ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara, uliofanyika April 7, 2025 katika Uwanja wa Sabasaba uloitishwa na mkuu huyo wa wilaya  kwa lengo la kujitambulisha kwa wananchi  na kusikiliza  kero zao.

KASSANDA amewapongeza wakazi wa wilaya  hiyo kwa mwamko walionao  kwenye  elimu, kwani kwa  wanafunzi waliotakiwa  kujiunga  na  kidato cha kwanza mwaka 2025, asilimia 98 ya wanafunzi wamesharipoti na kuanza masomo.

Sambamba na hayo amewataka wazazi na viongozi wa dini,  kusimamaia malezi yenye maadili kwa watoto ili kuwaepusha na tabia  hatarishi ikiwemo mapenzi ya Jinsia moja.

Katika mkutano huo wa hadhara, Mkuu wa wilaya KASSANDA amekabidhi mfano wa hundi  ya  shillingi million 148 ambazo ni  kati  ya  shilling million 545.5  ambazo zimetolewa kwa  vikundi 105 kupitia mikopo ya 10% iliyotolewa  na  halmashauri ya mji Masasi kwa mwaka  wa fedha  2024/2025.

Mkuu wa wilaya ya Masasi Bi Rachel Kassanda, akikabidhi mfano wa hundi ya Shillingi Million 148 kwa wawakilishi wa vikundi vya ujasiriamali. Picha na Godbless Lucius.