Mufindi FM

Wanaotegemea maji mto Ruaha wakumbukwa

16 July 2024, 21:11

Mbunge wa Jimbo la Mafinga Cosato Chumi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Itimbo katika ofisi ya kijiji, wakati wa kukabidhi mradi wa maji Julai 16, 2024. Picha na Hussein Nyalusi

MAFINGA.

Na Bestina Nyangaro
Takribani wananchi wapatao 3,200 wa kijiji cha Itimbo kata ya Rungemba halmashauri ya mji Mafinga wanatarajia kuondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kupata huduma ya maji ifikapo disemba mwaka huu 2024, ambapo mradi wa maji Itimbo unatarajiwa kukamilika.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mradi huo kwa mkandarasi, mbunge wa Mafinga mjini Cosato Chumi leo julai 16, makabidhiano ambayo yamefanyika kwenye kitongoji cha Geza Ulole, amesema kwa nafasi yake ataendelea kuisimamia serikali kutatua kero na changamoto za wananchi.

Sauti ya Chumi

Awali akisoma taarifa ya mradi Meneja wa wakala wa maji vijijini (RUWASA) Mhandisi Happiness Mrisho, amesema mradi huo utagharimu kiasi cha shilingi million 900 fedha za P for R na kutekelezwa kwa muda wa miezi 6 kwenye vitongoji 5.

Sauti ya Eng. Happiness Mrisho

Kwa upande wake mkandarasi wa mradi huo Eng. Chelesi ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Chelesi General Interprisess ameahidi kutekeleza mradi kwa wakati.

Sauti ya Eng. Chelesi

Diwani wa kata ya Rungemba Samwel Mwalongo, amewaonya wanufaika wa mradi huo kutojihusisha na vitendo vya wizi na uhujumu wa miundombinu jambo linaloweza kukwamisha mradi, huku baadhi ya wananchi wakiwashkuru viongozi kwa kuwawakilisha vyema.

Sauti ya Diwani na wananchi Itimbo