Radio Fadhila

Wanawake wenye kipato cha kawaida kujitoa kwa wahitaji

09/03/2026, 11:53

Bi Mariam kasembe akizungumza

Na Lilian Martin

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (ccm) wilayani Masasi Bi. Mariam kasembe amewapongeza wanawake waliojitoa kuhudumia watoto wenye mahitaji katika kituo kilichopo kata ya Napupa mtaa wa wapiwapi

Licha ya pongezi hizo Bi Mariam alimuomba Mbunge wa jimbo la Masasi ambaye ni waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleao ya makazi Mh. Leonard Akwilapo atakapopata nafasi aweze kutembelea katika kituo hicho na kuona jitihada zinazofanywa na wanawake hao

Mwenyekiti akizungumza

hata hivyo aliendelea kusisitiza juu ya upendo na malezi bora katika familia ili kupunguza wimbi la watoto wa mitaani

Akizungumza kuhusu malezi