Radio Fadhila

Wanawake wa kikristo waadhimisha siku ya maombi Duniani

07/03/2026, 09:30

Ni Bango lililotumika wakati wa maandamano ya maombi

Lengo kubwa la Wanawake hawa wa Masasi wakiungana katika maombi na wanawake wengine ni kukumbushana majukumu ya Wanamke katika maisha ya kila siku na kumtegemea Mungu katika nyakati zote ili jamii iwe sawa

Na Lilian Martin

Wanawake wa wakikristo kutoka Madhehebu Mbalimbali Wilayani Masasi wameungana kwa pamoja kuadhimisha siku ya Maombi Duniani huku kauli mbiu yao ikiwa ni “Tupeleke Mizigo”

Maadhimisho hayo yaliyofanyika Katika kanisa la Rc Magumuchila yaliyohudhuriwa na wanawake kutoka madhebebu mbalimbali yamelenga kuwakumbusha wanawake juu ya majukumu yao na kudumu katika maombi ili kuijenga jamii yenye kumjua Mungu

Wakati wa maadhimisho kanisa la Rc magumuchila

na kwaupande wake Mwenyekiti msaidizi wa umoja wa Wanawake Bi Veronika Mkwatile alieleza namna alivyo barikiwa na makutano hayo ya pamoja na wamama wenzake

Katibu msaidizi akizungumza

Sambamba na hayo Wanawake walikumbushana kuhusu kukemea maswala ya ukatili wa kijinsia na kuwaombea watoto katika jamii ili kuondokana na Wimbi la Ushoga