Radio Fadhila
Radio Fadhila
12 January 2026, 1:52 PM

Karibu kusikiliza kipindi maalumu ambapo mkuu wa wilaya ya Masasi bi. Racheal Kasanda amewaasa wazazi kuapeleka watoto shule na kuandikisha watoto darasa la awali katika umri mtahiki.
Katika mazungumzo yake na waandishi wa habari ametoa takwimu ya watoto wambao wameshaandikishwa na kuwataka wazazi kuwa na mwitikio mkubwa wa kuandikisha watoto kwa ajili ya kesho ya watoto.
Pamoja na hayo amewahimiza wazazi kufanya tathimini ya maisha yake kabla ya kumpeleka mtoto katika shule za kulipia kuepuka kumyumbisha mtoto.
