Radio Fadhila

Umaki watembelea shule ya Rondo, waunga mkono juhudi za taasisi

29 September 2025, 12:28 AM

Wa mama wakiwa na wanafunzi

Kutoa ni moyo si utajiri’, huu ni msemo unaofahamika sana na ukiwa na lengo la kukumbusha namna kutoa sehemu za Mali zetu kwa wenye uhitaji, hivyo wa mama hawa wamefanya kwa sehemu yako.

Katika kuendelea kuunga mkono jitihada za Taasisi za Elimu nchini wamama wa UMAKI Kanisa Anglikana mtaa wa lindi wamefanya ziara ya kutembelea shule ya rondo seminary na kuwapelekea zawadi wanafunzi shuleni hapo ikiwa imeambanata ,chakula pamoja na fedha kuajili ya kusapoti maendeleo ya shule.

Na kwaupande wake Mkuu wa Shule Bwn Linus Burian aliwashukuru wa mama wa Umaki kwa moyo wa kujitoa na kuona haja ya kuunga mkono maendeleo wa shule hiyo kwa kuwakumbuka watoto.

Wakufrahi pamoja na wanafunzia

Sambamba na kushukuru Mkuu wa shule aliwataka wazazi kuendelea kuwa mabalozi wazuri kuitangaza shule ya Rondo na kuwapeleka vijana wao katika shule hiyo kwa ajili ya elimu, maadili,na maarifa.