Radio Fadhila

NBC yamimina neema kwa wakulima Mtwara, Lindi

17 May 2025, 5:39 PM

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya  Wilaya  ya  Masasi  Alphaxad Etanga(aliyevaa fulana ya buluu), akiwa na wafanyakazi wa benki ya NBC wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya NBC Shambani. Picha na Godbless Lucius.

Kampeni ya NBC Shambani inatarajia  kuanza  rasmi juni 1 na itahitimishwa Julai 31 2025, ambapo wanaojihusisha  na biashara ya kilimo ambao ni wateja wa NBC, watakaokidhi vigezo watapatiwa  zawadi

Na Neema Nandonde

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), imezindua rasmi  kampeni ya NBC Shambani  msimu wa tatu,  inayolenga  kuwezesha na kufanikisha shughuli  za kilimo  kwa wadau  wote walioko kwenye mnyororo wa kilimo kwa mikoa ya Lindi  na Mtwara.

Uzinduzi huo umefanyika Mei 16, 2025 ambapo umewakutanisha viongozi wa  serikali, viongozi wa vyama vya msingi na ushirika, wafanyabiashara, maafisa ushirika na wakulima katika ukumbi wa Rock City Masasi huku kaulimbiu ya  kampeni  hiyo  ikisema “wekeza shambani ushinde”.

Akihutubia kabla ya uzinduzi huo,  mgeni rasmi  ambaye  ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya  Wilaya  ya  Masasi  Alphaxad Etanga, aliyemwakilisha  Mkuu wa Wilaya  ya  Masasi Rachel Kassanda, ameipongeza benki ya NBC kwa namna inavyofanya biashara kwa ukaribu na wakulima, huku akiitaka  kuendelea  kubuni njia mbalimbali za kuwainua wakulima.

Sauti ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya  Wilaya  ya  Masasi  Alphaxad Etanga

Akizungumza kwa niaba  ya  wakulima, Mwenyekiti wa  Chama  Kikuu  cha  Ushirika MAMCU Alhaj Azam Mfaume, ameipongeza benki ya  NBC kwa ushirikiano mkubwa wanaoutoa  kwa  wakulima,  huku akiwaomba kuendelea kuboresha  mifumo kwenye maeneo ya vijijini.

Sauti ya Mwenyekiti wa  Chama  Kikuu  cha  Ushirika MAMCU Alhaj Azam Mfaume
Baadhi ya wajumbe walioshiriki hafla ya Uzinduzi wa kampeni ya NBC Shambani msimu wa tatu. Picha na Godbless Lucius

Kwa upande  wake Meneja wa benki ya NBC Tawi la  Masasi Andrew Hossa, amesema kuwa   benki hiyo iko tayari kushirikiana na viongozi  wa vyama  vya  msingi na ushirika wilayani humo, ili kutatua changamoto mbalimbali za wakulima zinazokwamisha  kufikia malengo yao.

Sauti ya Meneja wa benki ya NBC Tawi la  Masasi Andrew Hossa

Kampeni ya NBC Shambani msimu wa tatu,  inatarajia  kuanza  rasmi juni 1 na itahitimishwa Julai 31 2025, ambapo  wanaojihusisha  na biashara ya kilimo ikiwemo wasambazaji wa pembejeo za kilimo, wakulima, wasafirishaji,, wavuvi, wafugaji ambao wana  akaunti  za NBC, watakaokidhi vigezo watapatiwa  zawadi ikiwemo pikipiki na  kompyuta mpakato.